Wednesday, June 19, 2013

*BENKI YA BADEA WAIPIGA JEKI SERIKALI YA TANZANIA JUMLA YA DOLA ZA KIMAREKANI 750 KUSAIDIA MIRADI YA MAJI NA KITUO CHA PAN AFRICAN

 Waziri wa Fedha Dk. William Mgimwa akiongea jambo na Mkurugenzi Mkuu wa Benki ya Kiarabu kwa Maendeleo ya Afrika  (BADEA) Abdelaziz Khelef  wakati wa utiaji saini wa makubaliano ya kuisaidia Tanzania dola za kimarekani 450,000/= kwa ajili ya miradi ya maji katika maeneo ya Mugango, Kiabakari na Butiama mkoani Mara na dola za kimarekani 300,000/= kwa ajili ya msaada wa kiufundi kwa ajili ya kusaidia kituo cha Hesabu cha Pan African kilichopo chuo Kikuu cha Dar es Salaam. Utiaji saini huo ulifanyika leo katika Hoteli ya Hyatt Regency jijini Dar es Salaam.
 Waziri wa Fedha Dk. William Mgimwa (kushoto) akimshukuru Mkurugenzi Mkuu wa Benki ya Kiarabu kwa Maendeleo ya Afrika  (BADEA) Abdelaziz Khelef  mara baada ya kumalizika  utiaji saini wa makubaliano ya kuisaidia Tanzania dola za kimarekani 450,000/= kwa ajili ya miradi ya maji katika maeneo ya Mugango, Kiabakari na Butiama mkoani Mara na dola za kimarekani 300,000/= kwa ajili ya msaada wa kiufundi kwa ajili ya kusaidia kituo cha Hesabu cha Pan African kilichopo chuo Kikuu cha Dar es Salaam. Utiaji saini huo ulifanyika leo katika Hoteli ya Hyatt Regency jijini Dar es Salaam.
 Baadhi ya maofisa kutoka Benki ya Kiarabu kwa Maendeleo ya Afrika  (BADEA) wakifuatilia  utiaji saini wa makubaliano ya kuisaidia Tanzania dola za kimarekani 450,000/= kwa ajili ya miradi ya maji katika maeneo ya Mugango, Kiabakari na Butiama mkoani Mara na dola za kimarekani 300,000/= kwa ajili ya msaada wa kiufundi kwa ajili ya kusaidia kituo cha Hesabu cha Pan African kilichopo chuo Kikuu cha Dar es Salaam. Utiaji saini huo ulifanyika leo katika Hoteli ya Hyatt Regency jijini Dar es Salaam.
 Waziri wa Maji Prof. Jumanne Maghembe akipongeza Waziri wa Fedha Dk. William Mgimwa (kushoto) mara baada ya kumalizika kwa    utiaji saini wa makubaliano ya kuisaidia Tanzania dola za kimarekani 450,000/= kwa ajili ya miradi ya maji katika maeneo ya Mugango, Kiabakari na Butiama mkoani Mara na dola za kimarekani 300,000/= kwa ajili ya msaada wa kiufundi kwa ajili ya kusaidia kituo cha Hesabu cha Pan African kilichopo chuo Kikuu cha Dar es Salaam yaliyofanyika leo katika Hoteli ya Hyatt Regency jijini Dar es Salaam. Kuli ni Mkurugenzi Mkuu wa Benki ya Kiarabu kwa Maendeleo ya Afrika  (BADEA) Abdelaziz Khelef.
Baadhi ya maofisa kutoka Benki ya Kiarabu kwa Maendeleo ya Afrika  (BADEA) wakifuatilia  utiaji saini wa makubaliano ya kuisaidia Tanzania dola za kimarekani 450,000/= kwa ajili ya miradi ya maji katika maeneo ya Mugango, Kiabakari na Butiama mkoani Mara na dola za kimarekani 300,000/= kwa ajili ya msaada wa kiufundi kwa ajili ya kusaidia kituo cha Hesabu cha Pan African kilichopo chuo Kikuu cha Dar es Salaam. Utiaji saini huo ulifanyika leo katika Hoteli ya Hyatt Regency jijini Dar es Salaam. Picha zote na Anna Nkinda-MAELEZO

*TRA IMETHIBITISHA KAMPUNI KUANZA KUUZA MASHINE ZA EFD

Mamlaka ya Kodi na MapatoTanzania (TRA) imeanza utekelezaji wa awamu ya pili ya mashine za kutolea stakabadhi zamauzo yaani Electronic Fiscal Device (EFD).
Awamu hii yapilii nawajumuisha wafanyabiashara wote ambao bado hawajasajiliwa na VAT na wenye mauzo ya zaidi ya Shillingi million 14 nakuendelea.
 
Mamlaka ya mapato (TRA) ilianzisha matumizi ya vifaavya utoaji wa risiti na invoices kwakila mauzo yatakayofanyika.
 
Kampuni ya PowerComputers niwasambazaji rasmi na maalum wa mashine za TRA.Tunatoa pia EFD Receipt Printer, Esign na mashine za ETR kwa wateja wote ambao wamesajiliwana TRA
Matawi yetu yapo Dar es salaam,(HQ),Mwanza, Arusha,Moshi,Mbeya ,Iringa,Tanga,Morogoro na Dodoma
Contact:
Mob: +255 656 760 050, 686 677 755, 767 084 602
Tel: +255 22 213 3039
Email: efd@powercomputers.net

*MAMA SALMA KIKWETE APONGEZWA KWA KUENDELEZA SOKA NCHINI

Mama Salma Kikwete
Na Anna Nkinda – Maelezo
Mke wa Rais Mama Salma Kikwete amepongezwa kwa jitihada zake za kuinua sekta ya michezo nchini   jambo ambalo limewafanya  vijana wengi kujipata ajira katika fani hiyo.
Pongezi hizo zimetolewa jana na Mwenyekiti wa Chama cha Mpira wa Miguu cha Mkoa wa Lindi  (LIREFA) Francis Ndulane wakati wachezaji wa timu ya Kariakoo ya mkoa huo walipozitembelea ofisi za Taasisi ya Wanawake na Maendeleo (WAMA)  zilizopo Ikulu jijini Dar es Salaam.
Ndulane alisema kuwa mchango unaotolewa na  Mama Kikwete umewapa hari na kuwatia  moyo vijana wengi na hivyo kuweza kuendeleza sekta ya michezo mkoani humo.
Alisema kuwa hapa nchini vijana wengi wana vipaji mbalimbali, lakini hawana watu wa kuwaendeleza, hivyo alimshukuru kwa jitihada zake za kuwaendeleza katika sekta hiyo na hivi sasa  wanaamini  kuwa wataweza kujiajiri na kuweza kuzisaidia familia zao.
Kwa upande wake Mama Kikwete ambaye pia ni Mwenyekiti wa Taasisi ya WAMA aliwapongeza wachezaji hao kwa juhudi kubwa wanayoifanya katika soka hadi kufikia hatua ya kushiriki ligi ya taifa ya mabingwa wa mkoa ngazi ya taifa na kufikia hatua ya nane bora.
Naye Mwenyekiti wa timu hiyo Abdalah Livemba aliwashukuru Mama Kikwete na Waziri wa Mambo ya Nje Bernard Membe kwa moyo walionao wa kuisaidia timu hiyo hadi kufikia  hapo ilipo.
Alimuomba kuwatafutia mdhamini ili awezkuwasaidia  kubeba mzigo mkubwa wa kuitunza timu hiyo ambao unaelekea kuwalemea.
Mama Kikwete aliikabidhi timu hiyo zawadi za  viatu pea 29, jezi seti mbili ambazo ni 32, mipira mitatu, pampu moja na  soksi  pea 16.
Timu ya Kariakoo inashiriki mashindano ya ligi ya mabingwa mkoa ngazi ya Taifa ambayo yalianza tarehe 12/6/2013 kwa kuzishirikisha  timu 28 kutoka nchi nzima wao wamebaki kati ya timu nane na leo wanapambana na Friends Rangers ya mkoa wa Dar es Salaam mchezo utakaofanyika katika uwanja wa Azam Complex uliopo Chamazi jijini Dar es Salaam.

*RAIS KIKWETE AREJEA NCHINI BAADA YA ZIARA YA KIKAZI NCHINI UINGEREZA

Rais Jakaya Mrisho Kikwete akisikiliza kwa makini maelezo aliyokuwa akipewa na Waziri Mkuu Ndugu Mizengo Pinda mara tu baada ya kuwasili kwenye uwanja wa ndege wa kimataifa wa Mwalimu Julius Nyerere akitokea nchini Uingereza. Rais Kikwete alirejea nchini jana tarehe 18.6.2013 usiku baada ya ziara ya kikazi nchini Uingereza. PICHA NA JOHN LUKUWI

Tuesday, June 18, 2013

*BAKWATA v/s ISTIQAAMA ZATOKA SARE, SHEIKH MKUU WA MKOA WA DAR, AL-HAD MUSSA, NYOTA WA MCHEZO

 Mshambuliaji na Nahodha wa timu ya Bakwata, Sheikh Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Al-had Mussa Salum (kulia) akimtoka beki wa timu pinzani ya Istiqaama ya Dar es Salaam, wakati wa mchezo wa kirafiki uliochezwa kwenye Uwanja wa Dar es Salaam Zuu, Kigamboni jijini mwishoni mwa wiki iliyopita. Katika mchezo huo timu hizo zilitoka sare ya 1-1.
 Kamanda kwa Polisi wa Kanda maalum, Suleiman Kova, akizungumza na waandishi wa habari wakati wa utambulisho wa mchezo huo mwishoni mwa wiki.
 Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Mecky Sadick, akimkabidhi Jezi, Nahodha wa timu ya Bakwata, Sheikh Al-had Mussa, wakati wa hafla ya kukabidhiwa vifaa vya michezo kwa ajili ya mchezo huo wa kirafiki uliochezwa mwishoni mwa wiki iliyopita. Katikati ni Nahodha wa timu ya Istiqaama, Saleh Omar Saleh.

Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Mecky Sadick, akimkabidhi Jezi, Nahodha wa timu ya Istiqaama, Saleh Omar Saleh, wakati wa hafla ya kukabidhiwa vifaa vya michezo kwa ajili ya mchezo huo wa kirafiki uliochezwa mwishoni mwa wiki iliyopita. Kushoto ni Nahodha wa timu ya Bakwata,  Sheikh Al-had Mussa,
 Sheikh Al-had Mussa, akionyesha umahiri wake wa kuchezea soka.
 Kikoso cha timu ya Bakwata.

*BALOZI SEIF AWAAGIZA WATAALAM WA UJENZI WA BARABARA KUHAKIKISHA UBORA WA BARABARA WANAZOJENGA NCHINI

  Msimamizi wa Mradi wa Bara bara tatu za Vijijini za Unguja kutoka Wizara ya Miundo Mbinu na Mawasiliano Mhandishi Suleiman Abdulla Ali akimpatia maelezo Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif Ali Iddi aliyetembelea mradi huo katika Barabara ya Cheju, Jendele – Kaebeona.
Mshauri Muelekezi waMradi huo Kutoka Kampuni ya Newtech Consulting Group ya Nchini Sudan El- Tayeb Rabah Mohammed akimuhakikishia Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif  ujenzi wa bara bara zenye kiwango katika mradi wa bara bara tatu za Vijiji za Unguja huko Cheju Wilaya ya Kati, Mkoa Kusini Unguja. Picha na Hassan Issa wa – OMPR – ZNZ.
*************************************
Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif Ali Iddi amewaagiza wataalamu wanaopata fursa za Ujenzi wa Bara Bara Nchini kuhakikisha bara bara wanazozijenga zinakuwa katika kiwango kinachokubakila Kimataifa ili ziwe na uwezo wa kudumu kwa kipindi kirefu.
Agizo hilo amelitoa wakati wa ziara fupi ya kukagua maendeleo ya ujenzi wa Bara bara ya Jendele-Cheju hadi Kaibona yenye urefu wa Kilo mita 11.741  ambayo ni miongoni mwa bara bara iliyomo  ndani ya mradi wa ujenzi wa bara bara tatu za vijijini katika Kisiwa cha Unguja.
Balozi Seif alisema wapo baadhi ya wahandisi wa ujenzi wa Bara bara wasio waaminifu ambao baadhi ya wakati hudiriki kuondoa njiani miradi ya ujenzi wa bara bara wanayopewa bila ya kuzingatia masharti na mikataba waliyoiridhia.
Alisema hali hiyo huleta kero kwa wafadhi wa miradi hiyo na mara nyingi kuyatia hasara Mataifa yenye miradi hiyo ambayo mengine yanashindwa kuihudumia Miradi husika kutokana na ufinyu wa uchumi wao.
“Baadhi ya  Makandarasi wamekuwa na tabia ya kuondosha njiani kazi wanazopewa za ujenzi tabia ambayo huwakera wafadhili wa miradi hiyo na kwa upande mwengine kuyaongezea mzigo Mataifa  yenye kusaidiwa ufadhili wa miradi hiyo “. Alisisitiza Balozi Seif.
Akizungumzia suala la fidia ya vipando, mali pamoja na majengo ya wananchi wanaoathirika na miradi hiyo Balozi Seif aliiagiza Wizara ya Miundo Mbinu na Mawasiliano Zanzibar kuwa makini ya baadhi ya watu wajanja wenye tabia ya kujipandikiza katika madai ya fidia hizo.
Alisema tabia hiyo ambayo hujichomoza mara kwa mara wakati wa uanzishwaji wa miradi tofauti katika maeneo mbali mbali Nchini imekuwa ikiitia hasara kubwa Serikali kwa vile haimo ndani ya jabeti iliyokubalika kwa pande zote mbili.
Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar aliipongeza Kampuni ya ujenzi wa Bara bara hiyo ya D.P Shapriya +Co. Ltd ya Dara es salaam kwa hatua iliyofikia ya ujenzi wa mradi huo licha ya kuchelewa kidogo kutokana na msimu wa mvua za masika.
Mapema Msimamizi wa Mradi huo wa Bara bara tatu za Vijijini Unguja kutoka Wizara ya Miundo Mbinu na Mawasiliano Zanzibar Mhandisi Suleiman Abdulla Ali alisema Serikali kupitia Wizara husika tayari imeshawalipa fidia wananchi wote waliohusika na ile bara bara ya Jendele- Cheju- hadi Kaebona.
Mhandisi Suleiman alimueleza Balozi Seif kwamba tathmini ya fidia imeshafanywa pia kwa bara bara ya Koani – Jumbi yenye urefu wa Kilo Mita 6.3 kwa kushirikiana na masheha wa shehia zinazopita bara bara hiyo na Wizara husika italipa fidia mara tuu fedha zitakapopatikana.
Alifahamisha kwamba ufinyu wa bajeti ya kazi za ujenzi wa Bara bara hizo za Vijijini Unguja umepelekea kutolewa kwenye mradi huo kwa Bara bara ya Kizimbani – Kiboje yenye kilo mita 7.
Msimamizi huyo wa mradi wa ujenzi wa bara bara hizo alieleza kuwa ujenzi wa kazi hiyo ulioanza mapema mwezi Januari mwaka huu wa 2013 umegharamiwa na Benki ya Maendeleo ya Kiislamu { Badea } kwa kushirikiana na SMZ  kwa kiasi cha  Shilingi za Kitanzania Bilioni 14,834,615,889.06/-.
Akitoa maelezo Mshauri muelekezi wa Mradi huo kutoka kampuni ya Newtech Consulting Group ya Nchini Sudan El-Tayeb Rabah Mohammed alisema kuwa mradi huo umepangwa kuchukuwa takriban miezi 17  hadi kukamilika kwake mwezi Mei mwaka ujao.
El – Tayeb alimuhakikishia Makamau wa Pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif kwamba ana matumaini makubwa ya kupatikana kwa kiwango kizuri cha ujenzi kitakachokidhi mahitaji yaliyokusidiwa kwa pande zote mbili.
Alieleza kuwa Wataalamu hao wa ujenzi wameshasafisha eneo la wastani wa Kilo mita 10 na kufanya kazi za kutengeneza Tabaka la Chini kwa wastani wa Kilo mita mbili kwa Bara bara ya Cheju –Jendele – Kaebona.
Wizara ya Miundo Mbinu na Mawasiliano Zanzibar ilitilianasaini Mkataba na Kampuni ya DP Shapriya + Co Ltd ya Dar es salaam kwa kazi za utekelezaji wa ujenzi wa Bara bara tatu za Vijijini Unguja mnamo tarehe 11 Septemba mwaka 2012.
Kukamilika kwa bara bara hizo  na hasa ile ya Cheju-Jendele- Kaebona kwa kiasi kikubwa itawaondoshea usumbufu wakulima wa zao la mpunga ambao walikuwa wakipata usumbufu kwa miaka kadhaa sasa.
Othman Khamis Ame
Ofisi ya Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar
18/6/2013.

*WACHEZAJI WA BONGO KUPATA ULAJI WA KUKIPIGA THAILAND NA BARANI ULAYA


KLABU ya Thai Port Football ya Thailand inatafuta wachezaji nchini Tanzania kwa ajili ya kucheza soka nchini humo na katika nchi nyingine barani Ulaya.

Kupitia kwa wakala wake, klabu hiyo imetuma taarifa kupitia Shirikisho la Soka Tanzania (TFF) ikitaka wachezaji wenye umri kuanzia miaka 15 hadi 28 kwa ajili ya kuwafanyia majaribio ambapo watakaofuzu watacheza nchini humo na katika klabu nyingine za Ulaya ambazo wana ushirikiano nazo.

Wachezaji wenye nia ya kufanya majaribio wanatakiwa kutuma taarifa za wasifu wao (CV) kwa klabu hiyo kwa njia ya emaili, wawe na pasi ya kusafiria pamoja na pasi ya mchezaji (player passport).

Wakala atapitia vitu hivyo, na kwa wachezaji atakaowahitaji atawatumia tiketi za ndege na viza kwa ajili ya kwenda kufanya majaribio nchini humo, na watakaofanikiwa kabla ya kusaini nao mikataba watawasiliana na klabu zao nchini (kwa wale wenye klabu).

Katika hatua nyingine, TFF inawashukuru washabiki kwa kujitokeza kwa wingi kwenye mechi ya mchujo ya Kombe la Dunia kati ya Taifa Stars na Ivory Coast (The Elephants) iliyochezwa juzi (Jumapili) kwenye Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam.
Mwitikio wa washabiki katika mechi hiyo ilikuwa ni moja ya chachu ya kiwango kilichoonyeshwa na Taifa Stars, kwani walishangilia mwanzo hadi mwisho licha ya kupoteza kwa mabao 4-2.

Ni matarajio utakuwepo mwitikio kama huo huo katika mechi ijayo ya Taifa Stars ya michuano ya Afrika kwa Wachezaji wa Ligi za Nyumbani (CHAN) dhidi ya Uganda (The Cranes) itakayochezwa Dar es Salaam kati ya Julai 12-14 mwaka huu. Stars itaingia tena kambini Julai 4 mwaka huu kujiandaa kwa mechi hiyo.

*HIVI NDIVYO ILIVYOKUWA MCHANA WA LEO JIJINI ARUSHA

Majira ya mchana hali ilikuwa kama hivi wakati Polisi walivyoanza kuwatawanya raia wanaodaiwa kuwa walikuwa ni wafuasi wa Chadema waliokuwa wamekusanyika kwa ajili ya kuaga miili ya marehemu waliokufa katika tukio la mlipuko wa bomu jijini humo hivi majuzi, ambapo Viongozi wa Chadema walianza kuwahutubia raia hao jambo ambalo tayari lilikuwa limeshazuiliwa na Jeshi la Polisi lililoeleza kuwa haliruhusu mkusanyiko wa aina yeyote kwa hivi sasa katika Jiji hilo, ili kupisha kazi ya uchunguzi wa matukio kadhaa yanayotokea ya milipuko ya mabomu inayotokea kila mara mkoani humo.

Baadhi ya Vijana nao walianza kuchoma matairi na magogo katikati ya barabara za jijini humo kama inavyoonekana pichani.

*BREAKING NEEEEWZ!!! MABOMU YARINDIMA ARUSHA KUTAWANYA WANAODAIWA WAFUASI WA CHADEMA, SUGU ANUSURIKA KUFA APATA AJALI AKIELEKEA ARUSHA

Habari zilizotufikia hivi punde chumba cha habari cha mtandao huu, zinasema kuwa Hali si shwari katika jiji la Arusha, ambapo hadi muda huu bado mabomu ya machozi yanaendelea kurindima baada ya Askari Polisi kuanza zoezi hilo kwa ajili ya kuwatawanya watu wanaodaiwa kuwa ni wafuasi wa CHADEMA, waliokusanyika katika viwanja vya Soweto wa ajili ya maombolezo ya watu waliofariki katika tukio la mlipuko wa bomu lililotokea mwishini mwa wiki iliyopita katika mkutano wa Chadema.

Aidha imeelezwa kuwa awali watu hao walizuiliwa kukusanyika eneo hilo na baadaye viongozi wa chadema walipofika eneo hilo walianza kuwahutubia wananchi waliokusanyika eneo hilo jambo ambalo lilizuiliwa huku vijana wakiimba nyimzo za maombolezo na za siasa, jambo lililowafanya askari kuchukua jukumu la kuwatawanya kwa mabomu ya machozi.

WAKATI HUO HUO:- habari zinaendelea kusema kuwa Mbunge wa Mbeya mjini JOSEPH MBILINYI Mr. ii, SUGU, amenusurika kufa baada ya kupata ajali eneo la Katesh Wilaya ya Hanang mkoa Manyara  wakati akiwa njiani kuelekea jijini ARUSHA.

Polisi Mkoa wa Arusha inawashikilia baadhi ya Viongozi wa CHADEMA, Mbunge wa Singida Mashariki Tundu Lisu na viongozi wengine kwa kuitisha mkutano usiokuwa halali ili kuondoa uvumi wa kuwa mbunge amefariki Dunia.

*SHOTI YA UMEME YAZUA BALAA MAENEO YA KARIAKOO MCHANA HUU, NI MOTOOOOOO


Moto huo uliozuka kutokana na shoti ya umememe ulisambaa ndani ya nyumba hii ambapo gari la zimamoto liliwahi katika eneo la tukio na kuanza kazi ya kuzima moto huo. Hadi sasa haijaweza kufahamika hasara iliyotokana na moto huo, uliowaka maeneo ya Kariakoo leo mchana.
Shoti ya umeme ilianzia hapa katika nguzo hizi ambapo cheche za moto ziliweza kusambaa. 
Sehemu ya raia wakishangaa ajali hiyo ya moto maeneo ya Kariakoo leo mchana.

*UJUMBE WA MFUKO WA VYOMBO VYA HABARI TANZANIA TMF WATEMBELEA OFISI ZA CHANGAMOTO

Afisa Uhakiki wa Miradi ya Mfuko wa Vyombo vya Habari Tanzania (Tanzania Media Fund TMF).Sanne Vanden Barg,(katikati)  akisisitiza jambo kwa waandishi wa habari wa magazeti ya Changamoto  na The Football wakati ujumbe wa TMF ulipotembelea katika ofisi za Ladyband zilizopo mtaa wa Daima  Mikocheni jijini Dar es Salaam. Kulia ni Afisa Miradi wa TMF Alex Kanyambo, na (kushoto) ni Naibu Mhariri Mtendaji wa Gazeti hilo Samson Kamalamo.

*RWIZA KUHUDHURIA SEMINA YA MAKAMISHNA CAF

Kamishna Alfred Kishongole Rwiza ameteuliwa na Shirikisho la Mpira wa Miguu Afrika (CAF) kuhudhuria semina ya makamishna itakayofanyika kuanzia Julai 6-7 mwaka huu katika makao makuu ya shirikisho hilo jijini Cairo, Misri.

Semina hiyo inashirikisha baadhi ya makamishna wa CAF walioko kwenye orodha ya makamishna ya shirikisho hilo kwa mwaka 2012-2014.

Rwiza ni mmoja wa makamishna wa CAF kutoka Tanzania, na mechi ya mwisho kusimamia ilikuwa ya Kombe la Shirikisho iliyochezwa Mei mwaka huu nchini  Msumbiji.

CAF tayari imeshamtumia tiketi Rwiza, na anatarajia kuondoka nchini Julai 4 mwaka huu kwenda Cairo kwa ndege ya EgyptAir.

*TFF YAWAPONGEZA MASHABIKI KWA KUIPA SAPOTI TAIFA STARS

SHIRIKISHO la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) linawashukuru washabiki kwa kujitokeza kwa wingi kwenye mechi ya mchujo ya Kombe la Dunia kati ya Taifa Stars na Ivory Coast (The Elephants) iliyochezwa juzi (Jumapili) kwenye Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam.

Mwitikio wa washabiki katika mechi hiyo ilikuwa ni moja ya chachu ya kiwango kilichoonyeshwa na Taifa Stars, kwani walishangilia mwanzo hadi mwisho licha ya kupoteza kwa mabao 4-2.

Ni matarajio utakuwepo mwitikio kama huo huo katika mechi ijayo ya Taifa Stars ya michuano ya Afrika kwa Wachezaji wa Ligi za Nyumbani (CHAN) dhidi ya Uganda (The Cranes) itakayochezwa Dar es Salaam kati ya Julai 12-14 mwaka huu. Stars itaingia tena kambini Julai 4 mwaka huu kujiandaa kwa mechi hiyo.

*SERIKALI YA MAPINDUZI ZANZIBAR YATUMA SALAMU ZA RAMBIRAMBI KWA MKUU WA MKOA ARUSHA

Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar imetuma salamu za rambi rambi kwa Mkuu wa Mkoa wa Arusha Mh. Magesa Mwilongo kutokana na vifo vya wananchi watatu wa Mkoa huo vilivyotokea kufuatia mlipuko wa bomu uliotokea  mwishoni mwa wiki katika viwanja vya Soweto Jijini Arusha.

Watu wasiopungua 70 waliripotiwa kujeruhiwa  wakati wa mripuko huo kwenye mkutano wa hadhara wa kampeni za uchaguzi katika Kata ya Soweto  wa Chama cha Demokrasia ya Maendeleo { Chadema }.

Katika Taarifa ya rambi rambi ya Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar  iliyotumwa kwa Mkuu huyo wa Mkoa wa Arusha  na kutiwa saini na Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif Ali Iddi alielezea kupokea kwa masikitiko na huzuni taarifa ya shambulio la kigaidi la bomu lililotokea tarehe 15 Juni mwaka 2013.

Balozi Seif alisema Taifa kwa mara nyengine tena limekumbwa na msiba wa njama za kigaidi zilizoua na kujeruhi raia wema wasio na hatia sambamba na tukio jengine linalofanana na hilo lililogharimu roho za wananchi wengine wakati wakiwa katika ibada Kanisani.

Balozi Seif alisema kwa niaba ya Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar, Wananchi na yeye binafsi anatuma salamu hizo za rambi rambi kutokana na maafa hayo na kuwaombea marehemu malazi pema na majeruhi wapone haraka ili waungane na wenzao katika ujenzi wa Taifa.

Halkadhalika Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar alisema Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar inaiunga mkono Serikali ya Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania katika jitihada zake za kupambana na ugaidi wa aina yoyote hapa Nchini.

Alieleza kwamba SMZ na Wananchi wa Zanzibar wako pamoja na wenzao katika kipindi hiki kigumu cha huzuni na maombolezo na kuwaomba wafiwa wawe na moyo wa ustahamilivu, uvumilivu na subra katika kipindi hichi.

Serikali ya Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania imeamua kutenga shilingi Milioni Mia Moja { 100,000,000/-} kama zawadi kwa kwa mtu ye yote atakayetoa Taarifa zitakazofanikisha kunaswa kwa mhalifu au watu wenye mtandao wa ulipuaji wa mabomu hapa Nchini.

Othman Khamis Ame
Ofisi ya Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar
18/6/2013.

*KOZI YA MAKOCHA MKOA WA DAR KUFUNGWA JUMANNE

Kocha Mkuu wa Twiga Stars, akitoa somo kwa Makocha wa Ngazi ya pili
kwa Vitendo wakati wa kozi hiyo inayoendelea ikitarajiwa kufungwa
rasmi junne ya wiki ijayo.

**************************************************
KOZI ya makocha wa ngazi ya pili (Intermediate) inayosimamiwa na Chama cha Mpira wa Miguu Mkoa wa Dar es Salaam (DRFA), inatarajiwa kufungwa Jumanne ijayo baada ya kudumu kwa wiki nne.Kozi hiyo ilianza Juni 3 mwaka huu kwenye Ukumbi wa Harbours Club, uliopo Kurasini chini ya Mkufunzi Rogasin Kaijage, ambaye ni Kocha wa timu ya Taifa ya Wanawake ‘Twiga Stars’ ambapo makocha mbalimbali pamoja na wachezaji wa zamani wamejitokeza kushiriki. 
Ofisa Habari wa DRFA, Mohamed Mharizo alisema kozi hiyo imekuwa na mafanikio na wanatarajia makocha walioshiriki katika kozi hiyo watakuwa na mchango mkubwa katika kuendeleza mpira wa miguu katika mkoa wa Dar es Salaan na Taifa kwa ujumla.

“Hadi sasa tunashukuru kuona tunafanikisha kozi hii ambayo wengi wameitikia wito, mwisho wa kozi hii ndio mwanzo wa kozi nyingine.

“Lakini haya ya kozi ya makocha ni moja ya majukumu ya Kamati ya Ufundi ya DRFA yaliyoainishwa katika Katiba, hivyo hili ni moja ya shabaha yetu na mengine mengi mazuri yanafuata,” alisema Mharizo.

Kozi hiyo ni ya kwanza kuendeshwa na DRFA tangu kuingia madarakani kwa uongozi mpya wa chama hicho Desemba 12, chini ya Mwenyekiti wake Almas Kassongo.
Baadhi ya makocha wakiwemo wachezaji wa zamani wakifuatilia 
mafunzo ya ukocha ngazi ya pili.
Kocha mkuu wa Twiga Stars, Rogasian Kaijage akitoa somo kwa 
makocha wanaoshiriki kozi ya ukocha ngazi ya pili ndani ya darasa 
kwenye Ukumbi wa Harbours Club, Kurasini.

*NDEGE NDOGO YA COASTAL ILIVYONUSURIKA BAADA YA KUPASUKA TAIRI ZANZIBAR JANA

 Ndege ndogo ya Coastal, ikiwa imeegeshwa pembeni mwa uwanja wa Ndege wa Zanzibar jana majira ya saa tano asubuhi iliponusurika kuingia porini baada yakupasuka tairi la kushoto wakati ikitua uwanjani hapo, na kuzua hofu kwa abiria waliokuwa ndani ya ndege hiyo, ambayo haikuweza kufahamika mara moja ilikuwa ikitua kutokea wapi. Katika ajali hiyo abiria wote walitoka salama na kuondolewa eneo hilo na gari la kubebea wagonjwa. 
 Gari la zimamoto likiwa pembeni ya ndege hiyo kujiandaa na dharula ambayo ingeweza kutokea uwanjani hapo...
 Gari la wagonjwa likiondoka na abiria waliokuwamo katika ndege hiyo.
Mafundi wakijitahidi kurekebisha hitilafu hiyo .......

*WABUNGE IDD AZAN NA HALIMA MDEE WAJIFUA KUWAKABILI JB NA WOLPER JULAI 7



Mbunge wa Kinondoni, Idd Azan akijifua na Mbunge wa Kawe, Halima Mdee, wanaojiandaa kupanda ulingoni Julai 7 mwaka huu kuzichapa na wapinzani wao, ambapo Azan anajiandaa kuzichapa na JB na Mdee akijiandaa kuzichapa na Wolper. 

*JE UMEWAHI KUSIKIA AU KUONA KISIMA CHA CHINI YA ARDHI? CHEK MAPICHA KAMILI

 Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akiingia shimoni wakati alipofika Mangapwani Kutembelea na kujionea Kisima cha Chini kwa Chini, kilichokuwa kikitumiwa na Wakoloni kupitishia Watumwa. Kisima hicho kilicho chini ya Ardhi huko ndani kuna Njia tatu, mbili zinatokezea Baharini na moja inatokezea katika moja ya Kijiji cha Mangapwani, ambayo hadi leo haijajulikana mwisho wa njia hiyo inapotokezea.
 Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akitoka shimoni kuangalia Kisima cha chini kwa chini kilichopo Mangapwani, ambacho kilikuwa kikitumiwa na Wakoloni kupitishia Watumwa. Kisima hicho kilicho chini ya Ardhi ndani kuna Njia tatu, mbili zinatokezea Baharini na moja inatokezea katika moja ya Kijiji cha Mangapwani, ambayo hadi leo haijajulikana mwisho wa njia hiyo inapotokezea.
 Ubao wa maelezo kuhusu historia ya Kisima hicho.
 Kamera ya Sufianimafoto kiwa ndani ya Kisima hicho chini ya ardhi.....
 Huu ni mlango wa kuingilia shimoni humo katiika Kisima hicho, ambao umetengenezwa na kuwekewa ngazi ili kuendana na wakati na kuwarahisishia wageni wanaofika kujionea maajabu yaliyomo ndani ya Kisima hicho, kilicho na njia tatu moja ikitokeza katika moja ya Kijiji kilichopo Mangapwani na mbili zinazotokea Baharini.
 Kisima hicho kilicho chini ya ardhi, ambacho siku nyingine hujaa maji na kufunika eneo hilo, na imeelezwa kuwa Kisima hiki ambacho maji yake hutumiwa na wananchi wa kijiji hicho hayakauki kwa mwaka mzima pamoja na kuwa maji hayo huchotwa na wananchi muda wote, ambao hutumia kwa kunya, kupikia na shughuli nyingine na maji hayo ni baridi yasiyo na chumvi.
 Askari waliosindikiza wageni kuingia katika Kisima hicho....
 Wageni wakishangaa Kisima hicho....
 Hii ndiyo njia moja inayoelekea Baharini, ambayo kwa sasa imeziba baada ya kuangukiwa na dongo kubwa lililoziba njia hiyo....Imeelezwa kuwa njia hizi zilikuwa zikitumiwa na Wakoloni wa Kiarabu kupitishia Watumwa, baada ya Kuingia Utawala wa Waingereza walikuwa wakipinga biashara ya utumwa, ambapo Waarabu waliamua kubuni njia nyingine ya kuendelea kufanya biashara hiyo kwa kificho, huku wakiwapitisha watumwa katika njia hiyo nyakazi za usiku na kuibukia Baharini na kukutana na Matajiri na kisha kufanya biashara na kuwapakia kwenye Majahazi yao na kuondokea huko, huku Majahazi yao yakitundikwa Bendera za Ufaransa na nyinginezo ili kukwepa kujulikana.
 Hii ndiyo njia ya kuingilia shimoni humo katika Kisima hicho......
 Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akitoka shimoni kuangalia Kisima cha chini kwa chini kilichopo Mangapwani, ambacho kilikuwa kikitumiwa na Wakoloni kupitishia Watumwa. Kisima hicho kilicho chini ya Ardhi ndani kuna Njia tatu, mbili zinatokezea Baharini na moja inatokezea katika moja ya Kijiji cha Mangapwani, ambayo hadi leo haijajulikana mwisho wa njia hiyo inapotokezea.
Rais Mstaafu wa awamu ya pili, Ali Hassan Mwinyi, akitoka shimoni kuangalia Kisima cha chini kwa chini kilichopo Mangapwani, ambacho kilikuwa kikitumiwa na Wakoloni kupitishia Watumwa. Kisima hicho kilicho chini ya Ardhi ndani kuna Njia tatu, mbili zinatokezea Baharini na moja inatokezea katika moja ya Kijiji cha Mangapwani, ambayo hadi leo haijajulikana mwisho wa njia hiyo inapotokezea.
 Maelezo ya Kisima hicho.....
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akisikiliza maelezo kutoka kwa Meneja na msimamizi wa Kisima cha Chini kwa Chini, Abdulwakir Zahro, wakati alipofika kutembelea na kujionea Kisima hicho cha Chini kwa Chini, kilichopo Mangapwani, Wilaya ya Kaskazini B, Mkoa wa Kaskazini Unguja juzi Juni 15, 2013. Kushoto ni Mlezi wa Tamasha la Asili la watu wa Mangapwani, Ali Hassan Mwinyi.